AJTC

Saturday 24 December 2016

UREMBO DADA WEWE WA MAVAZI NA WA MWILI KIUJUMLA.

Mavazi na Urembo


image
Pochi ni sehemu muhimu sana katika maisha ya mwanamke. Pochi zipo za aina, rangi, ukubwa na matumizi mbali mbali. Ni nadra sana kukutana na binti au mama anayetembea bila pochi, na kwa wengine maisha yao yote wanatembea nayo kwenye pochi.
Kuna vitu muhimu ambavyo ni lazima kila mwanamke akumbuke kutembea navyo kwenye pochi, na kuna vingine ni vyema kuwa navyo lakini sio lazima.
Muhimu
1. Pini
2. Sindano na uzi
3. Vifungo
4. Dawa yoyote ambayo unaitumia na kuihitaji
5. Kitambulisho
6. Pedi
7. Kalamu na notebook

Ukipenda
1. Perfume
2. Lip shiner / lip stick
3. Poda
4. Kitana
5. Khanga / mtandio
6. Kadi ya benki
7. Sandals kama unavaa viatu virefu

Mara nyingi wanawake tumekuwa tukijichukia na kujiona si wazuri wala hatupendezi kwa kuangalia muonekano wa nje. Unajiangalia na kujilinganisha na wengine na kuishia kuona mabaya (usiyoyapenda) na kuacha kuona jinsi Mungu alivyokuumba vyema na kukubariki. Utaona kuwa hauna nywele nzuri kama fulani, umenenepa/ kukonda sana, hauna elimu kama wengine, haujaolewa na mengine mengi.
Tambua hakuna mwanadamu aliye mkamilifu bali Yesu Kristo Bwana wetu ndiye atukamilishaye. Hivyo ulivyo ni wa thamani sana mbele zake na anakuhitaji uache kuangalia madhaifu yako bali umwangalie yeye ili aweze kukutumia. Jenga tabia ya kuhesabu baraka zako kila siku na utaona jinsi maisha yako yatakavyo badilika. Jione vile Mungu anavyokuona na acha kutumia vipimo vya wanadamu kutambua thamani yako.
Hivyo ulivyo Mungu anataka kukutumia, kwa elimu uliyonayo, kazi uliyonayo, nafasi yako hiyo hiyo uliyonayo, Mungu anakuhitaji. Unaweza kudhani kuwa ungekuwa na elimu zaidi, nafasi kubwa zaidi kwenye jamii, umeolewa, unakarama kama ya fulani basi ungemtumikia Mungu. Ukweli ni kwamba hivyo ulivyo unahitajika shambani mwa BWANA, kwa karama aliyokupa (kila mmoja wetu amepewa, nitafundisha juu ya hili siku zijazo). Anza sasa kumtumikia Mungu na utaona jinsi gani utabarikiwa na kuinuliwa zaidi na zaidi.
1 Korintho 15:10 Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo; na neema yake iliyo kwangu ilikuwa si bure, bali nalizidi sana kufanya kazi kupita wao wote; wala si mimi, bali ni neema ya Mungu pamoja nami.”

1Samweli 16:7 Lakini BWANA akamwambia Samweli, usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. BWANA haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje,bali BWANA hutazama moyo.
Mungu pekee ndiye anayeweza kuuona moyo wa mwanadamu, mwanadamu hawezi kuona moyo hivyo yeye yupata majiby yake pale anapoangalia mwonekano wa nje. Kutokana na hili basi ni vema wanawake wa kikristo tukawa na muonekano mzuri ili uwe ushuhuda mwema kwa wale wanaotutazama. Moyo mnyenyekevu na mwema huonekana katika muonekano wa nje, ni vyema tukajitahidi kuvaa vizuri, nadhifu na maridadi bila makwazo wala kujishushia thamani.
Muonekano mzuri ni muhimu sababu wewe ni kielelezo kwao waaminio na kwa wale wasioamini na kwa familia yako pia. Kwa wale walioolewa hakikisha muonekano wako haumfanyi mume wako akakosa heshima, vaa vile mume wako anavyopendezwa kuliko kuvaa ili kuwapendeza watu wengune.
2 Korinto 11:7b..Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume.
Pia kumbuka kuwa muonekano wako unaonyesha jinsi ulivyo, kama upo rafu rafu basi inaonyesha kuwa hata katika mambo yako mengine haujali, haipendezi mdada kwa na nywele zimefumuka au kuchakaa bila kuzitengeneza vizuri, au kuvaa nguo inayoonyesha sehemu kubwa ya mwili wako mfano kifua, mgongo au mapaja. Kwanza unajivunjia heshima na kumdharaulisha Mungu wako wa wale wanaokuona.
Vaa nguo inayokutosha vizuri, sio kubwa sana sio ndogo sana, hakikisha nguo ipo katika hali nzuri, sio unavaa sketi zipu imefungwa na pini au blauzi isiyo na baadhi ya vifungo. Pia ujue nguo ipi ni ya kuvaa mahali gani na kwa wakati gani, sio nguo ya kwenye sherehe ya usiku wewe unaivaa kanisani. Jitahidi kuuweka mwili wako katika hali nzuri, usiwe na harufu ya jasho wala nywele zisiwe na harufu yoyote mbaya. Tunza mwili wako maana ni hekalu la Roho mtakatifu. Jipende kwanza mwenyewe ili watu wengine nao waweze kupendezwa nawe.
Ubarikiwe.

Mikono ni mojawapo ya sehemu muhimu katika mwili wa mwanamke. Mikono hutumika kufanya shughuli zote za nyumbani kuanzia kupika, usafi, malezi n.k na isipotunzwa vizuri ni rahisi sana kuharibika na kupoteza mvuto wake wa asili. Urembo wa mikono sio lazima ufanyike saluni au kwa wataalamu, wewe mwenyewe unaweza kufanya hivyo kwa muda wako kwa gharama nafuu.
Vitu Vinavyohitajika
  • Pamba ya kutolea rangi kama umepaka rangi
  • Dawa ya kutolea rangi
  • Mashine ya kukatia kucha au mkasi mdogo
  • Tupa ya kucha (Nail file)
  • Brash ndogo ya mikono
  • Sabuni ya kunawia
  • Rangi ya kucha kama utapendelea
1.Kwa kutumia pamba na dawa ya kutolea rangi toa rangi yote kwenye kucha na hakikisha imetoka kabisa.
2. Kata kucha zako kwa urefu unaoutaka kwa kutumia ‘nail cutter’ au mkasi mdogo.
3. Lainisha ncha za kucha zako kwa kutumia tupa ya kucha, hakikisha unazisugua kuelekea upande mmoja ili kuepuka kucha kuvunjia. Kusugua kwa kwenda mbele na nyuma husababisha kucha kuvunjika upesi.
4. Kwa kutumia maji ya uvuguvugu na sabuni laini pamoja na brashi ndogo ya mikono, osha mikono yako vizuri na kuisugua  hasa sehemu za kucha.
5. Kausha mikono yako vizuri kisha paka losheni, hakikisha umepaka hadi kati kati ya vidole.
6. Kama utahitaji kupaka rangi, chukua pamba na remover na kutoa mafuta kwenye kucha zako kisha anza kwa kupaka rangi ya maji mpako mmoja na ikisha kauka ndipo upake rangi uliyoikusudia. Paka mpako wa kwanza acha ikauke kisha paka mpako wa pili na ukishakauka malizia na rangi ya maji ili kung’arisha na kuleta mvuto zaidi.
Tip: Kama kucha zako zimebadilika rangi kutokana na kupaka rangi mara kwa mara, loweka mikono yako kwenye maji yenye limao kwa dakika 5.
Kama hauna tupa ya kucha unaweza kutumia kiberiti ule upande wenye baruti.

Urembo na Mapambo
  • Bangili, hereni na mikufu unayoitumia mara kwa mara vinafaa vitundikwe kwenye stand maalumu mahali panapofikika kiurahisi mfano juu ya dressing table ili iwe rahisi kuvichukua na kutumia kila unapohitaji na kuzuia visishikane na hatimaye kuharibika.
  • Vito vya thamani viwekwe mahali salama kwenye container au box dogo zikizungushiwa kitambaa laini au sponji ili kuhifadhi thamani na mng’ao wake.
  • Hifadhi vitu vya aina moja pamoja, mfano dhahabu, silva, plastic, shanga, n.k ili iwe rahisi kujua kitu fulani kipo wapi kinapojitajika.
  • Hakikisha mikufu yote imefungwa vyema kuepuka kushikana na hatimaye kukatika.
Viatu
  • Viatu unavyovivaa mara kwa mara viweke kwenye ‘shoe rack’ mahali ambapo ni rahisi kuonekana kama ni kwenye korido au sehemu  yoyote rahisi kufikika.
  • Vipange viatu vyako kwenye shoe rack kufuatana na rangi, urefu wa kisigino, aina ya kiatu au matumizi.
  • Hakikisha viatu vyako ni vikavu na safi kabla ya kivihifadhi na hifadhi sehemu kavu isiyo na maji au unyevu.
  • Viatu ambavyo havivaliwi mara kwa mara kama vile vya kuvaa kwenye matukio maalinu ya usiku ni vyema vikihifadhiwa kwenye sehemu ya chini ya kabati.
Pochi
  • kama viatu pochi pia zinapendeza na pia kukusaidia kuokoa muda zikihifadhiwa kwa ukubwa, rangi, aina au matumizi.
  • Pochi unazotumia mara kwa mara weka kwenye stand maalumu na nyingine unaweza weka kabatini ili kupunguza wingi wa vitu kutundikwa kila mahali.
  • Pochi ndogo na wallet ziwekwe pamoja ndani ya droo au pochi kubwa ili kuepuka kupotelea ndani ya nguo au pochi nyingine.
Shalom
Dada Maria aliulizia kuhusu maternity wear ambazo zinaweza kuvaliwa ofisini na ukaonekana vizuri. Hapa kuna baadhi ya nguo ambazo zinafaa kuvaliwa ofisini kwa mtu ambaye hapaendelei kuvaa suruali. Kuna maternity sketi ambazo tumboni kunakuwa na belti kubwa la mpira la kukuwezesha kuvaa bila kupata tabu. Vile vile unaweza kuvaa magauni yenye mikono midogo mizuri au yasiyo na mikono na kisha kuvaa na koti dogo zuri au vijisweta vidogo na kukufanya ukaonekana mrembo na mwenye kupendeza.



Nadhani nitakuwa nimekusaidia, na wengine pia.
Ubarikiwe

Maternity Wear


Muda mrefu hatujaongelea mambo ya urembo na mavazi na leo nimeonelea tuangalie kidogo mavazi mbalimbali yanayopendeza kuvaliwa wakati wa ujauzito. Wengi tumezoea kuvaa nguo kubwa za vitenge zinazofika hadi chini, ni sawa kabisa lakini inapendeza ukiwa unavaa nguo za aina tofauti tofauti ambazo ni nzuri na hazikubani wala kukufanya ukaonekana mkubwa sana.
Hapa kuna baadhi ya nguo ambazo ukizivaa wakati wa ujauzito kwa kweli zinavutia, unaweza ongezea nakshi kama skafu, mtandio au hata kikoti kidogo na wewe mwenyewe ukajisikia vizuri.



NGUO IPI .....???????? IVALIWE WAPI?..................................

 
hebu leo tuongee kuhusu mavazi yetu hasa kina dada,
na hasa mavazi ya ofisini, na pia tuelimishane jamani, ni vazi gani la ofisini??? ni vazi gani la sherehe? ni vazi gani simple tu kwaajili ya nyumbani? na mavazi mengine meeeeeengi, TUTAKUWA TUKIANGALIA VAZI MOJA MOJA, NA LEO TUTAANGALIA JUU YA MAVAZI YA OFISINI TU!
Vazi gani hasa kwa wadada linafaa kuvaliwa ofisini???Tuambie uonavyo wewe
 
Unaweza kuvaa suti yeyote ile na ukapendeza,


si lazima suti tu, unaweza kuvaa hata kiblauzi chako simple skirt or trouser  na ukanoga tu


kama hawa huyu kavaa simple na amenoga, huyu nae suti pia amenoga


but naona kama vile suti zinapendwa sana ofisini,


unaonaeeee, mrembo huyo nimependa sana alivyovaa, BELT linakwenda na SKIRT yake, blauzi inaignia kidogo kwenye hiyo rangi ya skirt, umeona kiatu kileeeeee, (nimekipenda sana) basi pale kwa pembeni unapiga pochi black, We  inanoga hiyo, usipime!!!!!


mh! hapo sasa,!!!!!!!!!! si umeona tofauti iliyopo? si kwamba hajapendeza, kapendeza sana, lakini hii ni yakuvaa ofisini kweli?  sema na wewe, unaonaje? ofisini tuvae vipi wadada??? 
 
 

MAVAZI YA OFISINI

Habari  zenu Wapendwa, tumshukuru Mungu kwa kuiona tena siku hii ya leo, Mpenzi msomaji wa blog hii nakukalibisha kwa mara nyingine tena  usisite kutoa maoni yako  karibu sana.


Siku ya leo nitazungumzia kuhusu Mavazi ya ofisini  ni mavazi ya aina gani? siku ya leo utaweza kuyafahamu kwa undani zaidi , msomaji  mwavazi ya ofisini ni mavazi yanayo heshimika sana  mtu hawezi kuvaa jinzi au  suluali ya jinzi  kwa upande wa wasichana na wanawake hilo sio vazi la ofisini ingawa asilimia kubwa  wana vaa bora  amekwenda ofisini. Lakini ofisini ni sehemu muhimu sana kwa kuvaa vazi la heshima . haya ni baadhi ya mavazi ya ofisini  yanavyo leta muonekano tofauti.
Hili  ni moja wapo ya vazi la ofisini  linalo leta muonekano  tofauti kwa wavaji,pia rangi nyeupe na nyeusi ni moja wapo ya rangi zinazo leta mvuto na inapendeza kwa  kila mtu.




Rangi  ya  Blue na black ni rangi inayovutia sana kwenye mavazi ya suti   wadada wengi wanapenda sana kuvaa aina hii ya rangi.


Tumeweza kuyaona baadhi ya mavazi ya Ofisini yanavyo mfanya mtu awe tofauti hata mtu akivaa vazi la suti akawa anaenda sehemu nyingine tofauti na ofisini,anaonekana tu kama anafanya kazi. Kama tulivyo yaona mavazi ofisini  ni mavazi yanayo heshimiwa sana.





Muonekano tofauti



Mpenzi msomaji hayo yalikuwa ni mavazi ya ofisini, tuangalie upande mwingine wa Viatu pamoja mikoba inayo faa kuvaa kwenye mavazi ya ofisini na kumfanya mvaaji aonekane wa tofauti.


 Kwa upande wa  Viatu


 
inapendeza sana kwenye vazi la suti ukiwa umevaa vazi la black na white inavutia sana




Kwa wale wakinadada na wakina mama wanaoweza kutembelea viatu vya juu kama nilicho kuonesha hapo juu ni moja wapo ya kiatu kinacho pendeza sana , ila kina faa kwa wale wenye magari yao sio unapanda daradara ukiwa umevaa kiutu kama hiki.

Kwa upande wa pochi

  Ni pochi gani inafaa kuvalia nguo za suti












Hizi ni baadhi ya pochi zinazo leta mvuto kwa wanawake na wasichana  na kwa upande wa mavazi ya siti. Mpenzi msomaji wa blog hii utakuwa umeweza kuyaona mavazi ya ofisini pamoja na pochi na  viatu , msomaji endelea kuwa nami katika blog hii karibu sana


 hapo hupo msomaji ina pendeza sana

No comments:

Post a Comment